HABARI, BIASHARA, MUSIC, SIASA, MICHEZO,

Showing posts with label HABARI. Show all posts
Showing posts with label HABARI. Show all posts

Monday, 5 December 2016

Waziri Mkuu wa New Zealand John Key ajiuzulu

Waziri Mkuu wa New Zealand John Key ametangaza kwamba atajiuzulu wadhifa wake baada ya kuhudumu kwa miaka minane, akitaja sababu za kifamilia.
Alisema huo ndio uamuzi mgumu zaidi ambao amewahi kuufanya maishani.
"Sijui nitafanya nini baada ya hapa," alisema.
Bw Key, kiongozi anayependwa sana na watu, alikanusha taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba mkewe wa miaka 32 alikuwa amempa makataa.
Aidha, alisema hatawania muhula wa nne uchaguzi mkuu utakapofanyika mwaka 2017.
Makamu Waziri Mkuu Bill English anatarajiwa kuchukua majukumu ya uwaziri mkuu hadi chama cha National Party kikutane na kumteua waziri mkuu mpya.
Bw Key alitangaza kujiuzulu kwake kwenye kikao cha wanahabari cha kila wiki, ambapo alisema uamuzi wake umetokana na sababu za kinyumbani.
Alisema atang'atuka rasmi tarehe 12 Desemba.

Alisema kazi yake huhitaji kujinyima mambo mengi "kutoka kwa watu walio karibu sana nami" na kwamba watoto wake walikuwa "wameingiliwa sana".
"Ninachoweza kusema kwa sasa ni kwamba nilijitolea kwa kila kitu. Sikuacha chochote kwenye tangi."
Akimrejelea mkewe Bronagh, aliambia kipindi cha habari cha Newstalk: "Tulizungumzia hili na anafurahishwa na wazo langu kuwa nyumbani zaidi lakini hakukuwa na makataa."
Bw Key, ambaye zamani alifanya kazi Merrill Lynch kama mfanyabiashara wa sarafu za kigeni, alifikisha kikomo utawala wa Chama ch leba mwaka 2008 alipomshinda Helen Clark.
Alichaguliwa kwa muhula wa tatu kupitia chama cha National Party Septemba 2014.

Sunday, 27 November 2016

MWANDISHI WA KTN NCHINI KENYA AKAMATWA UGANDA

Mwandishi wa wahabari wa runinga ya KTN kutoka Kenya Joy Doreen Biira alikamatwa na kuzuiliwa na maafisa wa usalama nchini Uganda usiku wa Jumapili.
Vyombo vya habari zinasema Bi Biira alikamatwa pamoja na wengine watano kwa tuhuma za kupiga picha na video kuhusu operesheni ya maafisa wa usalama katika kasri la mfalme wa Rwenzururu na kuzichapisha kwenye mitandao ya kijamii.
Wanahabari na mashirika ya kutetea haki za kibinadamu wametoa wito kwa serikali kumwachilia huru.
Kitambulisha mada #FreeJoyDoreen (Mwachilie huru Doreen) kinavuma katika mtandao wa Twitter nchini Kenya.
Wanajeshi na polisi walivamia kasri hilo la Mfalme Charles Wesley Mumbere Jumapili.
Walinzi wake 46 waliuawa kwa mujibu wa polisi, na wengine 139 wakakamatwa.
Mfalme huyo alikamatwa pia na kuzuiliwa makao makuu ya polisi ya wilaya ya Kasese kabla ya kuhamishiwa mjini Kampala.
Gazeti la kibinafsi ya Monitor nchini humo linasema mfalme huyo anatarajiwa kukutana na Rais Yoweri Museveni baadaye leo.

Friday, 25 November 2016

FIDEL CASTRO AMEFARIKI DUNIA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 90

BREAKING NEWZ
Fidel Castro, kiongozi wa zamani wa Cuba aliyeongoza mapinduzi ya Kikomunisti, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90, kakake ametangaza.
"Amiri jeshi mkuu wa mapinduzi ya Cuba alifariki dunia mwendo wa saa 22:29 usiku huu (03:29 GMT Jumamosi)," Rais Raul Castro ametangaza.
Fidel Castro alitawala Cuba kama taifa la chama kimoja kwa karibu miaka 50 kabla ya kakake Raul kuchukua hatamu 2008.
Wafuasi wake walisema alikuwa ameirejesha Cuba kwa wananchi.
Lakini alituhumiwa pia kwa kuwakandamiza wapinzani.
Chini ya uongozi wa Fidel Castro, Cuba ilikuwa na uhusiano maalum na Afrika.
Katika miaka ya 1970 na 80, maelfu ya madaktari na walimu walikwenda Afrika na idadi sawa ya askari wa Cuba walipelekwa huko kuingilia kati migogoro na wakala wa vita baridi hasa nchini Angola.
Akitoa tangazo la kifo cha kakake, Rais Castro, aliyeonekana kuhuzunika sana, aliambia taifa kwenye tangazo la moja kwa moja kupitia runinga usiku kwamba Fidel Castro alikuwa amefariki na mwili wake utachomwa Jumamosi.
Kutakuwa na siku kadha za maombolezo ya kitaifa katika kisiwa hicho.
Raul Castro alihitimisha tangazo lake kwa kutamka kauli mbiu ya mapinduzi ya Cuba: "Twaelekea kwenye ushindi, daima!"
Kando na kuandika mara kwa mara gazetini, Fidel Castro alikuwa amestaafu kutoka kwenye siasa kwa muda mrefu, mwandishi wa BBC Will Grant aliyepo Havana anaripoti.
Mwezi Aprili, Fidel Castro alitoa hotuba nadra siku ya mwisho ya mkutano mkuu wa Chama cha Kikomunisti.
Alikiri kwamba alikuwa amezeeka sana lakini akasema maadili ya kikomunisti kwa Cuba bado yana maana na kwamba raia "watashinda".

NETANYAHU ADAI MOTO UNAOENDELEA KUTIKISA NCHI YAKE NI MBINU ZA KIGAIDI!




Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kuwa moto mkubwa ulioenea Magharibi mwa nchi hiyo huenda umesababishwa makusudi na yawezekana likawa ni tukio la kigaidi.
Akizungumza na wananchi katika mji wa Haifa ampapo zaidi ya maelfu ya wananchi waliondolewa kwenye makazi yao, amesema ni moja kati ya milipuko sita ya moto iliyowahi kutokea siku chache zilizopita ambapo maelfu ya makazi yameharibiwa kwa moto.
Moto huo unachochewa na hali ya ukavu unaosababisha moto kuenea haraka.
Nchi kadhaa zimetuma vikosi vya ndege vya zimamoto kusaidia kuzima moto huo ulionea pakubwa kwa muda mfupi.

Thursday, 24 November 2016






Huku maeneo mengi ya dunia yakihangaika na magereza yaliyojaa wafungwa kupita kiasi, Uholanzi ina tatizo tofauti. Uhaba wa wafungwa.
Katika kipindi cha chini ya miaka 19, magereza yamefunga shughuli zake na mengine zaidi yamepangwa kufungwa mwaka ujao. Ni vipi hili liliwezekana - na kwa nini baadhi ya watu wanafikiri ni shida?
Harufu nzuri ya kupendeza ya vitunguu inanukia, kupitia mlilango ya mahabusu na katika jengo zima. Jikoni wafungwa wanaandaa chakula chao cha jioni. Mwanamume mmoja aliyeko upande mmoja wa jiko anakata mboga.
"Nilikuwa na miaka sita ya kujifunza sasa nina uelewa zaidi wa shughuli hii!" alisema.
Ni kazi yenye kelele kwa sababu kisu kimefungwa kwenye nyororo ndefu iliyofungwa juu.
"Hawawezi kuchukua kisu hicho mikononi ," anasema Jan Roelof van der Spoel, naibu gavana wa gereza la Norgerhaven, lenye ulinzi mkali lililoko kaskazini mashariki mwa Uholanzi. "
"Lakini wanaweza kuazima visu vidogo vya jikonikama wakitoa vitambulisho vyao ili tufahamu ni nani ana nini."
Baadhi ya wanaume hao wamefungwa kwa kufanya makosa ya ghasia na wazo kwamba watembee na visu ni suala linalotia shaka. Lakini kujifunza kupika ni moja tu ya njia ambazo gereza husaidia wafungwa kurejea katika maisha ya kawaida mara baada ya kufunguliwa
"Katikka magereza ya Uholanzi tuanaangalia kila mmoja," anasema Van der Spoel.
"Kama mtu fulani ana matatizo ya mihadarati tunatibu hali yake, kama ni wenye hasira tunawapatia ushauri wa kudhibiti hasira zao , kama wana matatizo ya pesa tunawapatia ushauri nasaha. Kwa hiyo tunajaribu kuondoa kile kinachosababisha mtu afanye uhalifu . Mfungwa mwenyewe lazima awe na utashi wa kubadilika lakini njia yetu imewafaa sana. Kwa zaidi ya miaka 10 , kazi yetu imeboreka zaidi na zaidi.''
Wafungwa wanaofuata maelekezo hatimaye hupewa kifungo cha miaka miwili na msururu wa mafunzo katika mpango wa kuwarejesha katika hali ya kawaidi . Chini ya 10% hurejea gerezani baada ya kuachiliwa huru.
Hewa safi ni muhimu kwa hiyo wafungwa huruhusiwa kutembea wakisindikizwa hadi maktaba , kwenye kliniki ama mgahawa na hilo huwasaidia kuendelea na maisha ya kawaida punde wanapomaliza kifungo cha gerezani.
Muongo mmoja uliopita Uholanzi ilikuwa ni mojawapo ya nchi zenye kifungo cha muda mrefu zaidi barani Ulaya, lakini sasa inadai kuwa nchi yenye wafungwa wachache zaidi, yaani wafungwa - kati ya watu 100,000 , ikilinganishwa na wafungwa 148 Uingereza na Wales.
Lakini mpango wa kutoa ushauri nasaha si sababu pekee iliyosababisha kupungua kwa watu katika magereza ya Uholanzi - kutoka wafungwa 14,468 mwaka 2005 hadi wafungwa 8,245 mwaka jana - kiwango hicho kikiwa sawa na asilimia 43.
Kupungua zaidi kwa idadi hiyo mwaka 2005 kulisababishwa kwa sehemu kubwa na kuboreshwa kwa upekuzi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Amsterdam-Schiphol, ambako kulisababisha kubainika kwa idadi ya wauzaji wa mihadarati kukamatwa wakiwa wamebeba cocaine.
Angeline van Dijk, Mkurugenzi wa huduma za magereza nchini Uholanzi, anasema magereza sasa yanatumiwa kuwahifadhi wale ambao ni hatari sana kuachiliwa, ama wahalifu waliomo hatarini wanaohitaji usaidizi wakiwa ndani ya gereza.
"Wakati mwingine ni vyema kwa watu kukaa katika kazi zao, wakae na familia na kufanya adhabu kwa namna nyingine," anasema kulingana na uzoefu wake wa kazi hiyo.
"Tuna hukumu za muda mfupi za gerezani na kupunguza viwango vya uhalifu hapa Uholanzi, kwa hiyo hili linaacha magereza yetu kuwa matupu ."
Mojawapo ya gereza lililokosa watu liligeuzwa kuwa Hoteli ya kifahari kusini mwa mji wa Amsterdam, ni hoteli ya nne kwa kuwa ghali, ikipewa majina ... The Lawyer, The Judge, The Governor na The Jailer.
Lakini mengine yaligeuzwa kuwa vituo vya kuwapokea wahamiaji, na kutoa ajira kwa baadhi ya walinzi wa zamani wa magereza.
Azma ya kulinda ajira za magereza imetoa suluhu ya kushangaza - kuletwa kwa wafungwa wa kigeni kutoka nchi za Norway na Ubelgiji

Monday, 14 November 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo amekutana na Rais Mstaafu wa Afrika Kusini Mhe. Thabo Mbeki ambapo viongozi hao wawili wamezungumzia masuala mbalimbali kuhusu Umoja wa Afrika (AU).
Pamoja na kuzungumzia masuala yahusuyo Umoja wa Afrika, Rais Mstaafu Thabo Mbeki amempongeza Rais Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais Mstaafu Thabo Mbeki pia amempongeza Rais Magufuli kwa juhudi kubwa alizozifanya katika uongozi wa nchi kwa kipindi cha mwaka mmoja aliokuwa madarakani.
Kwa upande wake Rais Magufuli amemshukuru Rais Mstaafu Thabo Mbeki kwa kumtembelea na kufanya naye mazungumzo na pia amempongeza kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Usomi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Sunday, 6 November 2016

TANZIA!! SPIKA MSTAAFU WA BUNGE LA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AFARIKI DUNIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai kufuatia kifo cha Spika Mstaafu na Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Urambo Tabora Samwel Sitta.
Mzee Samwel Sitta amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Technical University of Munich Ujerumani alikokuwa akipatiwa matibabu tangu mwezi uliopita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai kufuatia kifo cha Spika Mstaafu na Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Urambo Tabora Samwel Sitta.
Mzee Samwel Sitta amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Technical University of Munich Ujerumani alikokuwa akipatiwa matibabu tangu mwezi uliopita.
Katika salamu hizo, Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Samwel Sitta na Taifa limempoteza mtu muhimu aliyetoa mchango mkubwa katika uongozi na maendeleo.
“Nitamkumbuka Mzee Sitta kwa uchapakazi wake, uzalendo wake na tabia yake ya kusimamia ukweli katika kipindi chote alichokuwa kiongozi katika ngazi mbalimbali za siasa na Serikali.
“Kupitia kwako Mhe. Spika naomba kutoa pole nyingi kwa Mke wa Marehemu Mhe. Magreth Sitta ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Urambo na familia nzima ya marehemu, Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wananchi wa Urambo Mkoani Tabora na watu wote walioguswa na msiba huu” amesema Rais Magufuli katika salamu hizo.
Dkt. Magufuli amesema anaungana na wafiwa wote katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo na amewaombea moyo wa uvumilivu na ustahimilivu.
“Namuomba Mwenyezi Mungu aiweke roho ya Marehemu mahali pema peponi, Ameni”
Taarifa imetolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU. Dar es Salaam

Thursday, 3 November 2016

IS Watamba kutouachia mji wa MOSUL

Kundi la Islamic State limetoa kanda ya sauti ambayo linasema kuwa ni kutoka kwa kiongozi wao Abu Bakr al-Baghdadi.
Ikiwa ni ukweli utakuwa ni ujumbe wa kwanza kutoka kwake katika kipindi cha mwaka mmoja, na huenda ukamaliza uvumi kuwa aliuawa.
Sauti hiyo inawataka watu nchini Iraq kulinda mji wa Mosul dhidi ya jeshi la Iraq, ambao linajaribu kuukomboa kutoka kwa wanamgambo wa Islamic State.
Mahala alipo Baghdadi hapajulikani. Baadhi ya maafisa wanasema kuwa huenda yuko ndani ya mji wa Mosul pamoj na wapiganaji wa Islamic State.
Haijabainika ikiwa saudi hiyo ni ya Baghdadi. Kuna uvumi kuhusu kuuawa kwake miaka iliyopita, ikiwemo mwaka uliopita wakati jeshi la Iraq lilisema kuwakuwa lilishambulia msafara wake.
Mosul ambayo ni ngome ya mwisho ya Islamic State nchini Iraq ndio mji Baghadadi alitangazia kujitawala miaka miwili iliyopita.
Mosul, the last IS urban stronghold in Iraq, is where Baghdadi declared a caliphate two years ago.
Abu Bakr al-Baghdadi au nee Ibrahim Awwad Ibrahim al-Badri, alizaliwa mwaka 1971 kwenye familia ya kusinni eneo la Samara nchini Iraq.
LEMBELI AMFUNGUKIA MAGUFULI KUHUSU MAJANGI! AWATAJA KWA MAJINA


VITA dhidi ya ujangili nchini imezidi kupata nguvu mpya baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira katika Bunge la 10, James Lembeli, kumuonyesha Rais John Magufuli mahala pa kuwanasa vigogo wa biashara hiyo haramu.


Akizungumza  jana, Lembeli alisema vita dhidi ya ujangili iliyopata msukumo mpya kutokana na agizo la Rais Magufuli alilolitoa wakati alipofanya ziara ya kushtukiza kwenye Wizara ya Maliasili na Utalii mwishoni mwa wiki, itapata mafanikio zaidi endapo orodha ya ‘majangili papa’ iliyomo kwenye ripoti ya ‘Operesheni Tokomeza’ itatua kwa Rais Magufuli na kufanyiwa kazi.

Akizungumzia maagizo aliyoyatoa Rais Magufuli, Lembeli alisema ni jambo jema, na kwamba kufanikiwa kwake kutatokana na utekelezaji wa ripoti ya ‘Operesheni Tokomeza’, aliyodai kwamba ilitaja mtandao wa vigogo muhimu pamoja na wafanyabiashara.

Juammosi iliyopita, Rais Magufuli alifanya ziara ya ghafla katika jengo la Wizara ya Maliasili na Utalii la Mpingo House jijini Dar es Salaam na kutoa maagizo kadhaa kuhusiana na vita dhidi ya ujangili. Siku hiyo Rais alimteua Jenerali mstaafu George Waitara kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa). 

Aidha, katika ziara yake hiyo, Rais Magufuli alisisitiza kuwa yuko nyuma ya vita dhidi ya ujangili na hivyo (operesheni) isimuache yeyote, kwa maana ya kuwakamata wahusika wa ujangili bila kujali cheo cha mtu, umri, jina, kabila, rangi wala dini yake. 

Alisema hayo baada ya kuona meno ya tembo 50 yaliyokamatwa, kuwaona watuhumiwa na pia kuelekeza kuwa anayo taarifa juu ya vikwazo mbalimbali kuhusiana na udhibiti wa vitendo hivyo.

UFAFANUZI KUHUSU ‘MAJANGILI PAPA’

Lembeli aliyekuwa akizungumza  baada ya kuulizwa maoni yake kuhusiana na kasi mpya katika vita dhidi ya ujangili, alisema wahusika wa vitendo hivyo ni baadhi ya vigogo waliokuwapo na waliopo hadi sasa serikalini.

Akifafanu, Lembeli alisema ni vigogo hao wasio waaminifu ndani ya Serikali ndiyo wanaolea biashara hiyo kwa namna mbalimbali, ikiwamo ya kuvujisha taarifa muhimu ambazo ndizo huwawezesha majangili kutekeleza uhalifu huo bila ya kuguswa na mkono wa dola.

Lembeli ambaye alikuwa Mbunge wa Kahama kabla ya kupoteza nafasi hiyo baada ya kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujaribu kutetea kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alisema anampongeza Rais Magufuli kwa hatua yake ya kutoa maelekezo muhimu katika vita dhidi ya ujangili.

Alisema anampongeza na kumuunga mkono kwa asilimia 100 Rais Magufuli, akidai kwamba anachokifanya sasa ndicho hasa kilichoelezwa kwenye ripoti ya ‘Operesheni Tokomeza’.

“Wakati ule, badala ya Serikali ya Awamu ya Nne kuifanyia kazi ripoti ile, wakaanza kuwashutumu watu kwamba siyo wana CCM,” alisema Lembeli.

Akitoa mfano, Lembeli alidai kuwa ndani ya ripoti hiyo, yumo kigogo mmoja wa polisi alisaidia kujaribu kutorosha meno ya tembo yaliyokuwa yamewekwa kwenye gari lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa dhidi yake.

“Huyo kigogo mpaka leo yupo. Kama Magufuli ataitumia vizuri ripoti ya Operesheni Tokomeza, vigogo hao wa ujangili watapatikana… na akitaka tumsaidie tutafanya hivyo. Asiwafuate wafanyabiashara peke yao. Ni kwa sababu wafanyabiashara hawa wanaongozwa na baadhi ya vigogo wa serikali,” alisema na kuongeza.

“Hakuna mfanyabiashara wa meno ya tembo anayeweza kufanikiwa kwenye hiyo biashara bila kushirikiana na watendaji wa Serikali. Wao ndiyo wanawapa mbinu zote.” 

Monday, 31 October 2016

JPM ZIARANI NCHINI KENYA



Rais wa Tanzania John Magufuli anatarajiwa kuanza ziara yake ya kikazi katika nchi jirani ya Kenya leo.
Kwenye ziara hiyo ya siku mbili, Rais Magufuli anatarajiwa kufanya mazungumzo na mwenyeji wake na pia kuzindua barabara mchepuko ya Southern By-pass iliyopo Jijini Nairobi.
Barabara hiyo, ambayo inaunganisha maeneo mbalimbali ya jiji la Nairobi kwa barabara za juu na chini, ni moja kati ya miradi mbalimbali ya ujenzi wa barabara ambayo imekuwa ikitekelezwa na serikali ya Kenya kupunguza msongamano wa magari katika jiji hilo kuu.
Rais Magufuli anatarajiwa kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta Jijini Nairobi majira ya saa nne asubuhi na baadaye kupokelewa rasmi na mwenyeji wake Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi ambako viongozi hao watafanya mazungumzo rasmi.
"Katika ziara hii Rais Magufuli anatarajiwa kutembelea kiwanda cha maziwa cha Eldoville kilichopo Karen Jijini Nairobi, na pia anatarajiwa kuzindua barabara mchepuko ya Southern By-pass iliyopo Jijini Nairobi," taarifa kutoka ikulu ya Tanzania imesema.
Ziara hiyo ya Rais Magufuli inajiri wakati ambao anakaribia kumaliza mwaka mmoja madarakani.
Katika kipindi hicho, hajakuwa akizuru sana mataifa ya nje na uhusiano kati ya serikali yake na serikali ya Rais Kenyatta umeonekana kuwa 'baridi kiasi'.
Tangu aingie mamlakani mwezi Novemba mwaka jana, amezuru tu Rwanda na Uganda.
Kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais, Dkt Magufuli alikuwa amehudumu serikalini kama waziri wa ujenzi.
Taarifa kutoka ikulu ya Tanzania inasema ziara yake imetokana na mwaliko wa Rais Kenyatta.
Kando na kutaka kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo mbili, wachanganuzi wanasema huenda Rais Kenyatta akaitumia kumpendekeza waziri wa mambo ya nje wa Kenya Bi Amina Mohammed ambaye anawania wadhifa wa mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika (AU).
Rais Uhuru Kenyatta atamkaribisha mgeni wake jijini Nairobi, baada ya Kenyatta kukamilisha ziara ya siku mbili huko Khartoum, alipokutana na Rais wa Sudan Omar Al- Bashir.

Thursday, 27 October 2016

Wanafunzi 11 waliokiri kufanya ngono na 

mbwa Arusha hawatashitakiwa

Wanafunzi wa kiume 11 wa shule za msingi Sombetini jijini Arusha wametuhumiwa kufanya ngono na mbwa eneo la mto Ngarenaro. Watoto hao ni wa miaka kati ya miaka saba na 11 wa darasa la tatu.
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Arusha , Charles Mkumbo amesema jeshi la polisi haliwezi kuwafungulia kesi wanafunzi hao ambao wamekiri kufanya vitendo hivyo mara kadhaa, kutokana na umri wao kuwa mdogo. Kamanda Mkumbo amesema………..
>>>’Kisheria, ili mtu aweze kushitakiwa na hilo kosa anapaswa angalau mtu mzima kuanzia miaka 13 na kuendelea, mtoto wa miaka 10 na kurudi nyuma kisheria hastahili kushtakiwa kwa jambo lolote alilolitenda la kijinai, mtoto miaka 11, 12 lazima ujilidhishe kwamba wakati anafanya kosa alikuwa na uelewa wa kutosha kwamba kosa hilo analolitenda ni kosa’
Aidha amesema jeshi hilo linawatafuta vijana waliowafundisha kufanya mapenzi na mbwa wakati watoto hao wakiendelea kupata ushauri wa kitaalamu

Wednesday, 26 October 2016

Watanzania milioni 1.4 wanaishi na VVU

Serikali imesema kuwa licha ya Mipango mikakati na mbinu madhubuti ambazo zimetekelezwa bado takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha maambukizi miongoni mwa makundi maalum na yale yaliyo katika hatari zaidi ya kuambukizwa VVU yapo juu.

Hayo yameelezwa katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto ambapo imesema ilianza kutoa huduma za VVU na UKIMWI kwa makundi hayo maalum tangu mwaka 2010 baada ya kufanya tafiti na kugundua kuwa kiwango cha maambukizi ya VVU kiko juu kwenye makundi hayo.
Serikali imeyataja makundi yaliyopo hatarini zaidi kwa maambuki hayo ni pamoja na wasichana na wavulana, walio katika umri wa balehe, watoto yatima na watoto walio katika mazingira hatarishi, wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao, wanawake wanaofanya ngono kinyume na maumbile, watu wanaotumia dawa za kulevya kwa njia ya kujidunga sindano.

Takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu 1,400,000 wanaishi na VVU nchini Tanzania ambapo, watu 839,574 wanapatiwa tiba ya dawa za kupunguza makali ya VVU zinazotolewa katika vituo ambapo takriban vituo 4,000 vilikuwa vinatoa huduma hiyo nchi nzima hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu (2016

Gambia nayo yatangaza kujiondoa katika mahakama ya uhalifu ICC

Serikali ya Gambia imesema kuwa itajiondoa kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC mara moja.
Hatua hiyo imekuja kutokana na madai kuwa ICC hushughulika na Waafrika pekee.
Maamuzi ya kujitoa katika mahakama hiyo yanafuatia baada ya Burundi na Afrika ya Kusini kutangaza kujiondoa
Rais wa nchi hiyo Yahya Jammeh amekua madarakani tangu mapinduzi nchini humo mwaka 1994.
Uchaguzi ujao unatarajiwa kufanyika desemba lakini mapema mwaka huu viongozi nane wa upinzani walikamatwa na kuhumiwa miaka mitatu jela kwa kuhusika katika maandamano ambayo hayakua na kibali.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty limesema kuwa maamuzi hayo ni sehemu ya muendelezo wa ukandamizaji wa haki za binadamu nchini Gambia.

Tuesday, 25 October 2016


Ukatili kwa Watoto wazidi kufanyika Arusha

Mkurugenzi wa Shirika la Women in Action for Development (WIA), Elizabeth Mosha.


Jiji la Arusha limeendelea kushuhudia vitendo vya ukatili dhidi ya watoto unaofanywa na walezi pamoja na wazazi ambapo watoto wawili wa familia tofauti wamethibitika kufanyiwa kitendo cha ubakaji na baba zao.
Imeelezwa kuwa kuendelea kwa vitendo hivyo vya kikatili kunachangiwa na baadhi ya madaktari kutofuata maadili ya kazi zao sambamba na kutochukuliwa hatua za kisheria kwa watuhumiwa wa vitendo hivyo.
Kwa Mujibu wa Bi Maria Thomas, ambaye ni mratibu wa idara ya elimu katika shirika linalo jihusisha na maendeleo ya wanawake na watoto yatima Women in Action for Development (WIA) Anaeleza jinsi walivyogundua kufanyiwa kitendo hicho kwa mtoto Janeth mwenye umri wa miaka 6 wakati akiwa shuleni.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Women in Action for Development (WIA), Elizabeth Mosha, amesema kuwa wataendelea kusimamia kesi hiyo mpaka mtuhumiwa atiwe hatiani ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaowafanyia vitendo hivyo watoto.
Mtuhumiwa aliyefanya kitendo hicho cha kikatili anayefahamika kwa jina la Jumanne Saidi mwenye umri wa miaka 59 mkazi wa kwa Morombo Jijini Arusha bado haijajulikana hatma yake huku jeshi la polisi likiendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo
Aidha katika tukio lengine la ukatili wa kijinsia kwa watoto, mtoto mwenye umri wa miaka 7 amefanyiwa kitendo hicho na baba yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Majimoto Huseni mwenye umri wa miaka 38 ambapo inaelezwa kuwa mama mlezi wa mtoto huyo kutokuwa na maelewano na mumewe kwa kipindi kirefu.
Tukio hilo ni la 5 kuripotiwa katika kituo cha Women in Action for Development (WIA).

Monday, 24 October 2016

SalymJuma>>>2sUPDATES Hukumu ya rufaa ya aliyekuwa mbunge wa Longido, Onesmo Nangole imeahirishwa hadi pale mkurugenzi wa uchaguzi pamoja na mwanasheria mkuu wa serikali watakapowekwa kwenye rufaa hiyo.******
******Awali mahakama kuu kanda ya Arusha ilitengua ubunge wa Onesmo Ole Nangole kutokana na kujaza matokeo ya ubunge kwenye fomu ya udiwani.


Ajira hizi apa! Jaribu bahati yako



MABAHARIA WALIO TEKWA SOMALIA 2012 WAACHIWA HURU


Kundi la mabaharia ambao waliachiliwa huru Jumamosi baada ya kuzuiliwa na maharamia kwa miaka mitano nchini Somalia walikula hata panya ili waishi, mmoja wao amemwambia Mwandishi wetu, kutoka Ufilipino amesema walikuwa wanapewa maji kidogo sana na walijihisi kama "wafu waliokuwa wakitembea" kufikia wakati wa kuachiliwa huru kwao.
Mabaharia hao walitekwa wakiwa kwenye meli mwaka 2012 kwenye pwani ya Ushelisheli na wakapelekwa Somalia bara na kuzuiliwa mateka.
Waliachiliwa huru Jumamosi. Taarifa zinasema waliokuwa wanawazuilia mateka walilipwa kikombozi.

Saturday, 22 October 2016

Kesi ya Akina Kitilya yatakiwa kuharakiswa!!!

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewataka mawakili wa Serikali kuharakisha upelelezi wa kesi inayomkabili Kamishna Mkuu wa zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitlya na wenzake.
Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Syprian Mkeha, upande wa Serikali ulikuwa ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Mutalemwa Kishenyi, wakati utetezi ukisimamiwa na Alex Mgongolwa.
Kishenyi alidai mahakamani hapo kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika hivyo aliomba mahakama iahirishe shauri hilo.
“Mheshimiwa leo (jana) kesi hii imekuja kwa ajili ya kutajwa pia tumepokea maombi kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuwa iahirishwe kwa kuwa Takukuru nao hawajakamilisha upelelezi wao,” alisema Kishenyi.
Upande wa utetezi ulilalamika na kudai kwamba kesi bado ipo gizani kwa sababu kila inapotajwa Serikali wanasema upelelezi haujakamilika.
“Ni takribani miezi sita sasa wateja wangu wapo mahabusu, naomba mawakili wa Serikali waharakishe suala hili,” alidai Mgongolwa.
Kutokana na hoja hiyo, mahakama ilipanga kesi hiyo itajwe tena Novemba 4, mwaka huu na washtakiwa walirejeshwa tena mahabusu.
Mbali na Kitilya, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 1996, Shose Sinare na aliyekuwa Mwanasheria wa Benki ya Stanbic, Sioi Solomon ambao wanakabiliwa na mashtaka mbalimbali likiwemo la utakatishaji wa fedha.
Mashtaka mengine ni kutumia nyaraka za kughushi na za uongo na kujipatia isivyo halali Dola milioni sita za Marekani sawa na Sh bilioni 12, pia katika tarehe tofauti kati ya Agosti, 2012 na Machi, 2013 jijini Dar es Salaam washtakiwa walipanga kwa ushirikiano na watu wengine kujipatia fedha kutoka serikalini kwa njia ya udanganyifu.
Pia ilidaiwa mahakamani hapo kuwa kati ya Agosti 2, 2012 katika Ofisi za Makao Makuu ya Stanbic Tanzania Limited zilizopo Kinondoni, Shose akiwa na nia ovu alighushi taarifa za maombi ya fedha katika Benki ya Standard.

Kwa mara ya kwanza washtakiwa hao walifikishwa mbele ya mahakama hiyo Aprili, mwaka huu.

Wednesday, 19 October 2016

IJUE SABABU YA SCOPION KUFUTIWA SHTAKA LILILOKUWA LIKIMKABILI


MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala mchana huu inatarajia kumfungulia shitaka jipya Salum Henjewele maarufu Scorpion baada ya shitaka la awali la unyang’anyi wa kutumia silaha kufutwa.
Awali Mahakama hiyo ililazimika kufuta shitaka hilo kufuatia maombi yaliyowasilishwa na Mwendesha Mashitaka, Munde Kalombola ambaye aliiomba mahakama hiyo kufutwa kwa shauri hilo mbele ya Hakimu Mkazi Adelf Sachore ambaye aliridhia maombi hayo baada ya upande wa mashtaka kutokuwa na nia ya kuendelea na shauri hilo.
“Kutokana na maombi yaliyowasilishwa na upande wa mashtaka, Mahakama imeliondoa shitaka hili kama ilivyoombwa kupitia kifungu cha 91 kifungu kidogo cha 1,” alisema Hakimu Sachore.

Kifungu hicho cha 91(1) kinampa mamlaka DPP kuliondoa shitaka hilo, Scorpion anatarajiwa kufunguliwa mashitaka mapya mchana huu.